• Nairobi
  • Last Updated April 30th, 2024 1:01 PM
Mahakama yatetea uamuzi wa kumtoza faini ya Sh2m aliyeitisha hongo ya Sh15m

Mahakama yatetea uamuzi wa kumtoza faini ya Sh2m aliyeitisha hongo ya Sh15m

Na BENSON MATHEKA

MAHAKAMA imetetea uamuzi wa kumtoza aliyekuwa meneja wa Mamlaka ya Ukusanyaji Ushuru (KRA), Robert Maina Ngumi faini ya Sh2 milioni kwa kuitisha hongo ya Sh15 milioni miaka sita iliyopita.

Uamuzi huo ulizua hisia kali miongoni mwa Wakenya wakishangaa jinsi mtu aliyeshtakiwa kwa madai ya kuitisha hongo ya Sh15 milioni alitozwa faini nafuu sana.

Hata hivyo, kwenye taarifa Alhamisi, idara ya mahakama imefafanua kuwa Bw Ngumi alikamatwa na wapelelezi wa Tume ya Maadili na Kupambana na Ufisadi (EACC) kabla ya kupokea pesa alizokuwa akidai kama hongo.

“Siku aliyokamatwa, aliwekewa mtego na maafisa wa EACC. Pesa halisi alizopokea zilikuwa dola za Amerika 1,100 sawa na Sh110,000 za Kenya. Noti zingine zilikuwa feki, kwa hivyo kesi ilikuwa kuhusu Sh110,000,” imesema taarifa ya mahakama.

Mnamo Jumatano, Mahakama ya kusikiliza kesi za ufisadi ilimhukumu Bw Ngumi kufungwa jela miezi 18 akishindwa kulipa faini hiyo.

EACC pia imethibitisha kuwa Ngumi alikamatwa kabla ya kupokea pesa zote alizoitisha kama hongo ili aweze kupunguzia kampuni moja kodi iliyotakiwa.

“Pesa alizookea Bw Ngumi zilikuwa zimewekwa alama na EACC na ndizo alizopatikana nazo alipokamatwa. Hakupokea pesa zozote,” EACC ilisema kwenye taarifa.

You can share this post!

Watatu wafariki, wanane wajeruhiwa kwenye ajali eneo la...

COVID-19: Visa 147 vipya, wote ni Wakenya

adminleo