• Nairobi
  • Last Updated May 11th, 2024 7:15 PM
Mapato kutoka kwa Wakenya walio ughaibuni yaongezeka

Mapato kutoka kwa Wakenya walio ughaibuni yaongezeka

Na BERNARDINE MUTANU

Serikali imepokea ongezeko la mapato kutoka kwa wananchi wanaoishi nje ya nchi wakati wa robo ya mwanzo ya 2018.

Mapato hayo yaliongezeka maradufu katika kipindi hicho ikilinganishwa na 2017. Katika muda kati ya Januari na Machi, wananchi wanaoishi nje ya nchi waliwasilisha nchini Sh20.99 bilioni zaidi.

Hivyo, katika kipindi hicho, serikali iliweza kupokea Sh64.4 bilioni kutoka kwa wananchi hao.

Ukuaji huo unatokana na hali ya uchumi iliyoimarika na kuondolewa kwa adhabu na Mamlaka ya Kutoza Ushuru nchini (KRA).

Habari hii ni kwa mujibu wa mchanganuzi wa uchumi wa Stanbic Jibran Qureishi.

Mwaka wa 2017, wananchi wanaoishi nje ya nchi walituma nyumbani Sh197.12 billion, ukuaji wa asilimia 13.09 ikilinganishwa na 2016 ambapo walituma Sh174.30 bilioni.

  • Tags

You can share this post!

Korti yaagiza mshukiwa wa wizi wa magari akimbizwe...

Faini ya Sh500,000 kwa kumeza hongo ya Sh2,500

adminleo