• Nairobi
  • Last Updated April 30th, 2024 8:55 PM
Miguna adai amezuiwa kuabiri ndege ya kutoka Frankfurt hadi Nairobi

Miguna adai amezuiwa kuabiri ndege ya kutoka Frankfurt hadi Nairobi

Na IBRAHIM ORUKO

WAKILI Miguna Miguna ambaye anatarajiwa Kenya baada ya kukaa nchini Canada kwa muda karibu ya mwaka mmoja amedai kwamba amezuiwa kuabiri ndege ya kutoka uwanja wa ndege wa Frankfurt, Ujerumani hadi Nairobi kwa sababu ya kikwazo cha Kenya.

Nayo Kenya kupitia kwa msemaji wa serikali Cyrus Oguna inasema kwamba wakili huyo yuko huru kurejea, likiwa ni hakikisho la Rais Uhuru Kenyatta na kwamba Wizara ya Masuala ya Kigeni inalishughulikia suala hilo la ‘kizuizi’.

Alitarajiwa Jumanne asubuhi kuabiri ndege ya shirika la Lufthansa lakini akazuiwa; ikiwa ni pigo kwake ikizingatiwa alikuwa amekamilisha awamu ya kwanza kwa kusafiri kutoka Canada hadi nchini Ujerumani ili aunganishe safari hadi jijini Nairobi.

Katika ‘kizuizi’ ofisi ya Rais ilikuwa imeonya shirika dhidi ya kumsafirisha wakili huyo hadi nchini Kenya au taifa lolote la Bara la Afrika.

 

Tunaandaa habari kamili…

You can share this post!

Mzozo wa Iran kuumiza Kenya

Gor, Tusker wajikita kileleni Homeboyz, Ulinzi wakipaa

adminleo