• Nairobi
  • Last Updated May 1st, 2024 9:11 AM
Miili ya maafisa wawili kutoka Bomet yapatikana Homa Bay

Miili ya maafisa wawili kutoka Bomet yapatikana Homa Bay

Na BARACK ODUOR

MIILI ya watu wawili wanaoaminika kuwa wafanyakazi wa serikali ya Kaunti ya Bomet, ilipatikana imetupwa katika Kaunti ya Homa Bay Jumatatu jioni.

Polisi wanachunguza vifo hivyo baada ya kupata miili hiyo katika kijiji cha Kanga Omuga, kaunti ndogo ya Rachuonyo Kusini, ikiwa na majeraha mbalimbali.

Miili hiyo ilipatikana imetupwa kichakani katika barabara iliyo kwenye mpaka wa kaunti za Homa Bay na Kisii.

Kulingana na chifu wa eneo hilo, Bw Joshua Otieno Oluso, wakazi waliona gari aina ya probox likitupa miili hiyo kisha likaondoka kwa kasi kuelekea mahali pasipojulikana.

Kamanda wa Polisi katika Kaunti ya Homa Bay, Bw Maris Tim, alisema wawili hao walitambuliwa kama Bw Bernard Kimutai Kirui na Bw Rotich Kipkorir Dominic.

Kamanda huyo wa polisi alisema wanaume hao walikuwa wamepeleka pesa kwa benki kugharamia kesi inayoendelea mahakamani katika kaunti. Alisema risiti za benki na pesa zilipatikana kando ya miili hiyo.

 

You can share this post!

Wakenya kuhesabiwa idadi Agosti 2019

TAHARIRI: Heko Spika Muturi kukataa ombi tata

adminleo