• Nairobi
  • Last Updated May 1st, 2024 5:01 PM
Mlipuko watokea Mogadishu

Mlipuko watokea Mogadishu

ABDULKADIR KHALIF

Mlipuko mkubwa ulisikika kwenye mji mkuu wa Somalia Mogadishu mapema Jumamosi.

Ripoti zilisema kwamba mnamo saa moja na nusu asubuhi kuna gari liliangukia ukuta karibu na bandari na likalipuka.

Maelezo yalikuwa machache huku maafisa wa wakushughulikia dharura wakishughulikia hali hiyo, lakini polisi walisema kwamba watapeana habari zaidi baadaye.

Kufikia sasa hakuna kikundi kilichojitokeza na kudai kuhusika na mlipuko huo wa asubuhi.

Wafanyavibarua wengi hutembea bandarini asubuhi na mapema kutafuta kazi.

  • Tags

You can share this post!

CORONA:  Hali si hali baadhi ya wakazi wa mijini wakihamia...

Mwanamume avua nguo kupinga mkewe kupokonywa kiti

adminleo