• Nairobi
  • Last Updated May 1st, 2024 10:08 PM
Msiwapasue watoto wa jinsia mbili, madaktari waonywa

Msiwapasue watoto wa jinsia mbili, madaktari waonywa

Na Steve Njuguna

MADAKTARI wametakiwa kutokuwa na haraka ya kuwafanyia upasuaji watoto walio na jinsia mbili; uke na uume.

Wanaharakati wa kutetea haki za kibinadamu wanasema kuwa watoto hao wanafaa kuachwa hadi wakati wa kubaleghe ndiposa wafanyiwe upasuaji.

Afisa wa Tume ya Kitaifa ya Haki za Kibinadamu (KNCHR), Amos Wanyoike alisema kuwa mhusika anaweza kuonekana msichana lakini wakati wa kubaleghe anabadilika kuwa mwanaume.

“Tumekuwa tukiona madaktari wakikimbilia kuwafanyia upasuaji watoto hao ili wawe wa kiume au kike. Upasuaji huu haufai. Madaktari wanafaa kungojea hadi wakati wa kubaleghe,” akasema Bw Wanyoike.

Afisa huyo aliwataka wabunge kufanyia mabadiliko Sheria kuhusu Usajili wa Watu ili kuhakikisha kuwa watu walio na jinsia mbili wanatambuliwa.

Afisa wa KNCHR tawi la Nyahururu Noreen Wewa alisema kuwa wameanzisha kampeni ya kuhamasisha jamii kuhusiana na watu wenye jinsia mbili.

Ripoti ya sensa iliyotolewa a Shirika la Takwimu nchini (KNBS) ilionyesha kuwa kuna watu 1,524 wenye jinsia mbili nchini Kenya.

 

You can share this post!

Polisi wanyakwa wakimeza hongo

Polisi wasifiwa kwa juhudi za kuzima uhalifu

adminleo