Habari Mseto                                                
                                            
                                        Mwanamume avua nguo na kujitia kitanzi baada ya kugombana na mkewe
 
                                                    
                                                        Mayai ya kuku waliolishwa mishayiri. PICHA|SAMMY WAWERU                                                         
                                                Na FLORAH KOECH
WAKAZI wa kijiji cha Chemogoch, Eldama Ravine, Kaunti ya Baringo wameshangazwa na kisa cha mwanaume mmoja aliyevua nguo zote kabla ya kujitia kitanzi katika shamba lake baada ya kugombana na mkewe.
Kulingana na maafisa wa usalama na chifu wa eneo hilo, Patrick Rono, 34, baba ya watoto watatu alifika nyumbani kutoka sokoni na kupata mkewe ametoroka kitendo ambacho inashukiwa kilimfanya kujiua.