• Nairobi
  • Last Updated May 18th, 2024 8:57 PM
Mwili wa msichana ambaye mamake alijirusha mtoni wapatikana

Mwili wa msichana ambaye mamake alijirusha mtoni wapatikana

Na GEORGE MUNENE

MWILI wa msichana mwenye umri wa miaka mitano ambaye alizama kwenye mto Nyamidi, Kaunti ya Kirinyaga na mamake umepatikana Jumapili.

Kisa hicho kilichosababisha mauti ya dogo huyo na kilichoshangaza kilitokea mnamo Jumamosi na mwili wa mamake nao bado haujapatikana.

Kamanda wa Polisi John Wachira alisema mwili wa mtoto huyo ulipelekwa katika hifadhi ya maiti huku mwili wa mamake nao ukiendelea kutafutwa.

Mwanamke huyo alijificha na akiwa amemfunga mwanawe mgongoni alijitumbukiza kwenye mto Nyamidi ambao umefurika na kuvunja kingo zake.

  • Tags

You can share this post!

Mahangaiko ya wasafiri katika barabara ya kuunganisha Kenya...

Koome ampelekea Ruto majina 20 ya majaji wapya walioteuliwa...

T L