Natembeya sasa ahudumia wakazi kutoka Kaunti Ndogo baada ya kufungiwa nje na korti
GAVANA wa Trans Nzoia, George Natembeya, siku ya Jumatano, alirejea kazini huku akikabiliwa na mashtaka katika mahakama ya Maadili na Kupambana na Ufisadi jijini Nairobi.
Gavana huyo alianza kuhudumu kutoka afisi za Kaunti Ndogo ya Kiminini ili kutii agizo la mahakama akionekana kukwepa mtego wa kusalia kazini.

Hii imehamisha kitovu cha mamlaka kiotomatiki kutoka kwa ofisi yake rasmi kutoka katikati mwa Jiji huku akichukua majukumu yake rasmi kutoka afisi ya Kaunti Ndogo ya Kiminini.
Jumanne iliyopita wakati wa uamuzi wake wa dhamana, Mahakama ya Kupambana na Ufisadi jijini Nairobi ilimzuia gavana Natembeya kuhudumu kutoka ofisi zake kwa siku 60.
Hii ni baada ya Gavana huyo kukamatwa nyumbani kwake Nairobi huku nyumba yake ikivamiwa huko Milimani na maafisa wa upelelezi wa EACC kabla ya kufikishwa mahakamani.