• Nairobi
  • Last Updated May 13th, 2024 9:17 PM
Pombe yaua tena Kirinyaga na kugeuza wawili kuwa vipofu

Pombe yaua tena Kirinyaga na kugeuza wawili kuwa vipofu

NA GEORGE MUNENE

MTU mmoja alifariki na wengine wawili kupoteza uwezo wa kuona baada ya kunywa pombe yenye sumu katika kijiji cha Kandongu, Kaunti ya Kirinyaga, Jumatano usiku.

Inaaminika kuwa watatu hao walikunywa pombe iliyowekwa kemikali yenye sumu hasa baada ya kuanza kutapika na kulalamikia maumivu ya tumbo.

Walikimbizwa na majirani katika zahanati ya Kandongu hali zao zilipozidi kuwa mbaya, lakini mmoja wao alifariki akipokea matibabu.

“Tumempoteza mtu mwingine aliyetambulika kama Paul Mwai kwa pombe yenye sumu, hali ni mbaya,” alisema mmoja wa wakazi, Bi Jane Muthoni.

Bi Muthoni alisema, Bw Mwai alikuwa jirani yake na kwamba alikuwa miongoni mwa waliompeleka hospitalini.

“Nilikuwa nyumbani nilipopata taarifa kuwa hali yake imekuwa mbaya baada ya kunywa pombe na mara moja tulimkimbiza hospitalini ila akaaga dunia,” alisema.

Wakazi waliojawa na hasira walishutumu polisi kwa kushindwa kukabiliana na watu wanaouza pombe yenye sumu katika eneo hilo.

Kisa hiki kinajiri siku chache baada ya watu wengine 15 kuangamia baada ya kunywa pombe yenye sumu katika kijiji cha Kangai.

  • Tags

You can share this post!

Kenya kurejelea kupeleka majanichai Tanzania baada ya...

Kocha Gervais Hakizimana: Kielelezo cha urafiki wa kufa...

T L