• Nairobi
  • Last Updated May 2nd, 2024 7:50 AM
Sababu ya hoteli za Norfolk kufunga biashara Kenya

Sababu ya hoteli za Norfolk kufunga biashara Kenya

NA ADONIJAH OCHIENG

Kampuni ya hoteli za Fairmont Norfork Nairobi imetangaza kufungwa kwake kwa ghafla na kuwafuta wafanyakazi wote kutokana na kuzorota kwa biashara kuliosababishwa na mikakati hasi iliyowekwa kuzuia kusambaa kwa virusi vya corona.

Kulingana na barua aliyotoa meneja wa hoteli hizo Mehdi Morad ya Mei 27, kutokuwa na uhakika kuhusu mkondo utakaochukuliwa na sekta ya hoteli katika janga hili la corona kumelazimisha kukatisha mikataba yao na wafanyakazi.

Wafanyakazi watapokea barua zao za kutamatisha huduma zao kufikia Juni 5. Hoteli nyingi za kifarahi zinazotegemea utalii na makongamano kupata faida zinapitia wakati mgumu wakati huu wa janga la corona.

Mwezi Machi  hoteli za Nairobi kama vile Ole Sereni, Tribe Hotels na Dusit D2 zilisimamisha shughuli zake serekali ilipoweka mikakati ya kutotangamana na kusimamisha usafiri ili kuzuia kusambaa kwa corona.

Amri ya kutotoka au kuingia nchini imeathiri sana sekta ya utalii iliyoletea nchi Sh163.56 milioni mwaka uliopita.

You can share this post!

Wandani wa Ruto wamiminika kwa Mudavadi

LISHE NA VINYWAJI: Ni faida zipi mtu anapata kwa kunywa...

adminleo