• Nairobi
  • Last Updated May 1st, 2024 7:53 AM
Shirika lataja Reggea kama kikwazo kwa elimu ya watoto

Shirika lataja Reggea kama kikwazo kwa elimu ya watoto

Na CHARLES LWANGA

SHIRIKA la kijamii la kupambana na mihadarati mjini Malindi limesemaa miziki ya kisasa aina ya Reggea inachangia katika uzorotaji wa viwango vya masomo miongoni mwa vijana na kusababisha takriban vijana 300 kuacha masomo kila mwaka.

Bw Edison Mwabonga, ambaye ni afisa wa miradi katika shirika la Omar Project mjini Malindi, linalohudumia waathiriwa wa mihadarati katika Kaunti ya Kilifi, Tana River na Lamu alisema vijana wengi huanza kuvuta bangi jinsi wanavyoshuhudia katika nyimbo hizo kabla ya kuacha masomo.

“Mara nyingi vijana huiga wanachotazama katika televisheni kama vile kuvuta bangi, uhalifu na uasherati ambao huwafanya kuwa watundu,” aliambia Taifa Leo.

Baadhi ya wasanii maarufu wa Raggae kama vile marehemu Bob Marley, Joseph Hill na wengineo kutoka Jamaica wamesifia sana bangi na hata kuvuta katikati ya nyimbo zao.

Vilevile, haya yameletwa na disko matanga na uongezekaji wa maskani za kunywa pombe maarufu kama mangwe ambazo pia zimeongeza visa vya uhalifu Mnarani na Maweni.

Kamishna wa Kaunti Magu Mutindika pamoja na Gavana Amason Kingi wamepiga marufuku disko matanga kama njia mojawapo ya kuwawezesha vijana kuhudhuria shule na kupunguza mimba za mapema.

Bw Mwabonga ambaye amehudumia shirika hilo tangu mwaka wa 1990 alisema vijana 900 wenye umri wa miaka 18 hadi 37 walioathiriwa na mihadarati wanapokea matibabu ya Methadone katika hospitali ya Malindi.

“Vijana wengine 2,446 katika Kaunti ya Lamu, Tana River na Kilifi wanapokea sindano za kuwasaidia kuepuka mihadarati wanayotumia kujidungia dawa ya methadone,” alisema.

Alisema pia baadhi ya vijana hao walikuwa wemejiingiza katika sekta ya utalii na ukahaba kabla ya kuokolewa na shirika hilo kutokana na dawa za kulevya.

Kwa upande wake, Bw Khamid Mudaris, ambaye ni mpangaji maalum katika Shirika la Omar Project alisema upatikanaji wa mihadarati hizo kama vile miraa, mugoka na bangi ndio chanzo cha ongozeko la ujambazi na mimba za mapema.

You can share this post!

Joho ataka awamu ya pili ya SGR iahirishwe

Wabunge waapa kuangusha pendekezo la ushuru wa mafuta

adminleo