• Nairobi
  • Last Updated May 5th, 2024 5:50 AM
Taabani kwa kujaribu kulaghai kampuni ya bima

Taabani kwa kujaribu kulaghai kampuni ya bima

Na RICHARD MUNGUTI

DEREVA mmoja alishtakiwa Alhamisi kwa kujaribu kuilaghai kampuni ya bima Sh380,000 akidai alihusika kwenye ajali iliyohusisha magari matatu.

Bw Antony Maina Nyambura alishtakiwa mbele ya hakimu mkuu katika mahakama ya Milimani Nairobi Bw Francis Andayi.

Alidaiwa alijaribu kuilaghai kampuni ya bima ijulikanayo Resolutions iliyoko jijini Nairobi.

Pia alikabiliwa na shtaka lingine la kutoa habari za uwongo kwa Konstebo Charles Nyambane kwa alihusika kwenye ajali katika barabara ya Souther Bypass inayounganisha barabara kuu ya Mombasa na ile ya Thika mjini Ruiru.

Mshtakiwa alikana mashtaka mawili na kuachiliwa kwa dhamana ya Sh200,000

  • Tags

You can share this post!

Kesi ya tatu ya sakata NYS kuanza Februari 2019

Wabunge wapinga wakulima kupigwa msasa kabla ya kulipwa

adminleo