• Nairobi
  • Last Updated May 3rd, 2024 10:50 AM
Tandaza ataka wakazi Dongo Kundu wafidiwe

Tandaza ataka wakazi Dongo Kundu wafidiwe

Na Fadhili Fredrick

WAKAZI zaidi ya 256 kutoka vijiji sita katika eneobunge la Matuga, watakaoathirika na ujenzi wa awamu ya tatu ya barabara ya kisasa ya Dongo Kundu, bado hawajafidiwa.

Mbunge wa eneo hilo, Bw Kassim Tandaza, sasa anataka serikali iwafidie waathiriwa hao kabla ya mradi kuanza.

Alisema licha ya orodha hiyo kupewa mamlaka husika miaka minne iliyopita, waathiriwa hao hawajafidiwa mashamba na mimea yao.

“Tayari mwanakandarasi wa Kichina yuko eneo la ujenzi na wakazi walioathirika bado hawajapokea fidia yoyote,” akasema.

Alisema wale wanaopaswa kulipwa kwa ardhi na mali zao ni pamoja na wanakijiji kutoka Mkumbi, Tuliani hadi kiijiji cha Kibundani na waathiriwa wengine pia.

Pia anataka wenyeji kupewa kipaumbele katika nafasi za ajira katika mradi huo.

  • Tags

You can share this post!

Kalonzo ageuka mtetezi sugu wa Uhuru mlimani

Yaibuka wakazi hulisha mifugo ndani ya mbuga ya Tsavo

adminleo