• Nairobi
  • Last Updated April 28th, 2024 12:38 PM
TANZIA: Nyota wa zamani wa timu ya taifa raga Allan Makaka afariki

TANZIA: Nyota wa zamani wa timu ya taifa raga Allan Makaka afariki

Na GEOFFREY ANENE

KENYA imeamkia habari za kuhuzunisha Jumamosi baada ya kumpoteza nyota wake wa zamani wa timu ya taifa ya raga ya wachezaji saba kila upande Allan Makaka Shisiali katika ajali mbaya ya barabarani iliyotokea saa sita usiku.

Makaka, ambaye alipeperusha bendera ya Kenya katika Kombe la Dunia 2005 mjini Hong Kong na Jumuiya ya Madola 2006 mjini Melbourne nchini Australia, alikuwa katika gari ndogo alipogonga lori lililokuwa limesimama kwenye barabara ya Mombasa Road kutoka nyuma.

Mchezaji huyu wa zamani wa klabu za Ulinzi na Kenya Harlequin alizaliwa mnamo Juni 28 mwaka 1982.

Alisomea katika Shule ya Msingi ya Mumias Boys kabla ya kujiunga na Shule ya Upili ya Musingu katika Kaunti ya Kakamega na kisha kupata digrii katika Chuo Kikuu cha USIU katika eneobunge la Kasarani katika Kaunti ya Nairobi.

Wakati wa kifo chake, Makaka ambaye alichezea Kenya jumla ya mechi 57 na kuifungia miguso 28 kwenye Raga ya Dunia, alikuwa meneja katika Shirika la Habari la Royal Media Services.

Mwili wake umepelekwa katika chumba cha kuhifadhia maiti cha Montenzuma kusubiri mazishi.

You can share this post!

KURUNZI YA PWANI: Elungata aelezea Wapwani haja ya...

BURUDANI: Amefuata asili ya upande wake wa nchi jirani...

adminleo