• Nairobi
  • Last Updated May 21st, 2024 8:55 PM
Waandamana kulalamikia kusitishwa kwa ujenzi wa barabara

Waandamana kulalamikia kusitishwa kwa ujenzi wa barabara

NA CHARLES LWANGA

Wakazi wa Malindi wameandaa maandamano ya kulalamikia kusimamishwa kwa ujenzi wa barabara inayofadhiliwa na Benki ya Dunia inayogharimu Sh67 milioni eneo la Mtangani, Kaunti ya Kilifi.

Wakazi hao wakiongozwa na madiwani Kadenge Mwathethe (Shela),  Edward Kazungu Dele (Sabaki) na David Kadenge Dadu (Malindi mjini), walisema kwamba walishangazwa na jumuiya ya wafanyabiashara wakazi wa Malindi ambao walienda kortini ili kuzuia kujengwa kwa barabara hiyo.

“Jumuiya hiyo ya wanabiashara walioenda kortini ili kuomba kusimamishwa kwa ujenzi wa barabara hiyo hawana haja na maitaji ya  wananchi ,”alisema bw Kadenge wananchi wamekuwa wakigoja barabara hiyo kwa miaka mingi kwa  watu wachache kusimamisha mradi huo”.

Hii ni baaada ya Jumjiya ya wafanyabiashara ikiogozwa na kikundi cha Malindi Progressive wwlfare Assocatio Pamoja na KNCCI walienda kortini kusimamisha ujeenzi wa barabara hiyo.

  • Tags

You can share this post!

Aliyenaswa na CCTV akiiba kwenye gari akamatwa

Mwanamke afariki baada ya kulala chumba kimoja na shemeji...