Habari Mseto                                                
                                            
                                        Wafungwa sita waliokuwa wametoka hospitalini wahusika kwenye ajali
 
                                                    
                                                        Wafungwa, polisi wa magereza wahusika kwenye ajali Homa Bay. Picha|George Odiwuor                                                    
                                                NA GEORGE ODIWUOR
WAFUNGWA sita na polisi watano wa magereza wamejeruhiwa kufuatia ajali ya barabarani iliyotokea mjini Homa Bay Jumanne alasiri.
Ajali hiyo ilitokea wakati karandinga la polisi wa magereza lilipopoteza mwelekeo na kuanguka huku likilalia upande mmoja.
Wafungwa hao walikuwa wameugua na wakati ajali hiyo ilipotokea, walikuwa wanarejeshwa jela la Rachuonyo kutoka hospitalini.
Waliojeruhiwa wamekimbizwa katika Hospitali ya Rufaa ya Homa Bay kwa matibabu.