• Nairobi
  • Last Updated April 28th, 2024 9:50 AM
Yaibuka Igathe anafaa zaidi kwa sekta ya benki

Yaibuka Igathe anafaa zaidi kwa sekta ya benki

Na BERNARDINE MUTANU

Aliyekuwa Naibu Gavana Nairobi, Bw Polycarp Igathe amerejea kwa sekta ya benki kwa kishindo.

Hii ni baada ya kuteuliwa na Benki ya Equity kama Afisa Mkuu wa Biashara (CCO), baada ya kuona kwamba anafaa zaidi kwa nafasi hiyo na wala si siasa.

Bw Igathe alijiuzulu kama naibu wa gavana mapema mwakani baada ya kutofautiana na Gavana Mike Sonko.

Benki hiyo inatarajiwa kumtangaza kama msimamizi wa wajibu huo wakati wa mkutano wa wawekezaji Alhamisi.

Alipojiuzulu, Bw Igathe alisema alikuwa amekosa kupata uaminifu wa mkubwa wake (Gavana Sonko), hivyo hakuweza kufanya kazi vizuri.

You can share this post!

Mkakati mpya wa kupunguza ada ya umeme

Ugali ghali wabisha

adminleo