Habari

Achani aahidi kuendeleza vita vya mihadarati

Na CECE SIAGO June 28th, 2025 Kusoma ni dakika: 1

GAVANA wa Kwale Fatuma Achani amehimiza vijana eneo hilo kujitenga na matumizi au ulanguzi wa dawa za kulevya, akiwataka wajihusishe na maendeleo yatakayowakuza kiuchumi.

Akizungumza jana wakati wa maadhimisho ya siku ya kimataifa ya kupambana na matumizi na ulanguzi wa dawa za kulevya, Bi Achani alionya vijana dhidi ya kutumia dawa hizo.
Aidha, alidokeza kuwa serikali ya kaunti imejitahidi kunasua vijana kutoka kwa uraibu huo.
“Tumeshirikiana na washikadau mbalimbali na tumefanikiwa kuokoa vijana zaidi ya 1,500 kutoka kwa janga la matumizi ya mihadarati, kupitia kwa kituo cha urekebishaji tabia cha Kombani,” Bi Achani alieleza.
Kamishna wa Kaunti ya Kwale Stephen Orinde alisema serikali ya kitaifa na ya kaunti zitaendelea na jitihada hizo ili kunasua vijana zaidi, huku akirai jamii kuwakumbatia wale waliorekebika ili kuzuia unyanyapaa ambao unaweza kuwafanya watumbukie tena katika uraibu wa mihadarati.