• Nairobi
  • Last Updated May 4th, 2024 10:15 PM
Mahakama yasikia kilio cha Ruto

Mahakama yasikia kilio cha Ruto

NA SAM KIPLAGAT

MAHAKAMA ya Rufaa imeruhusu serikali kuendelea kukata ushuru wa nyumba za gharama nafuu hadi pale itatoa uamuzi wake mnamo Januari 26, 2024.

Mwanasheria Mkuu Justin Muturi alifika kortini na kunyenyekea mbele ya mahakama hiyo kwa niaba ya serikali ambapo aliiambia kwamba ushuru huo ulikuwa tayari umesaidia kubuni nafasi za ajira 120,000.

Soma Pia: Ruto ainyenyekea mahakama aruhusiwe kukata ushuru wa nyumba

Majaji walioruhusu serikali kuendelea kukata ushuru huo ni Lydia Achode, John Mativo, na Mwaniki Gachoka.

“Hali iendelee jinsi ilivyo kwa sasa hadi uamuzi kuhusu kesi hii utakapotolewa,” wamesema majaji hao.

Mwanaharakati Okiya Omtatah aliwasilisha kesi ya kupinga ushuru wa nyumba ambao wafanyakazi hutozwa asilimia 1.5 ya mishahara yao, akisema kwamba ni ushuru wa kiubaguzi.

Mnamo Novemba 28, 2023, Mahakama Kuu ilibatilisha ushuru huo, lakini ikasema inaipa serikali hadi Januari 10, 2024, kukata rufaa.

  • Tags

You can share this post!

Hofu simba wenye njaa wakizurura ovyo vijijini

Nassir: Matibabu ya bure ni kwa watoto wa 001 pekee

T L