Habari za Kitaifa

Uhusika wa Orengo katika kikosi cha mawakili wa Bunge wapingwa na Gachagua

Na BENSON MATHEKA October 16th, 2024 Kusoma ni dakika: 1

MAWAKILI wawili wandani wa Raila ambao ni viongozi waliochaguliwa, wamejiunga na kesi ya kumtimua Naibu Rais Rigathi Gachagua wakiwakilisha Bunge la Kitaifa katika kikao cha Seneti.

Wakili James Orengo ambaye ni Seneta wa Siaya na mbunge wa Rarieda Otiende Omollo wameungana na, Paul Nyamodi, Erick Gumbo, Muthomi Thiankolu, Moses Kipkogei, Peter Wanyama, Ken Melly, Mwangi Kang’u, George Murugara, Samwel Chepkonga, John Makali na  Zamzam Mohamed kuwakilisha Bunge la Taifa.

Bw Murugara, Bw Chepkonga, Bw Makali na Bi Mohammed pia ni wabunge.

Upande wa Bw Gachagua unaongozwa na Wakili Paul Muite, Elisha Ongoya, Tom Macharia, Swanya Victor, Ndegwa Njiru, Faith Waigwa, Amos Kisilu, John Njomo, George Wandati Andrew Muge, Julia Omwamba, Eric Naibei na Willis Echesa.

Tayari, mawakili wa Bw Gachagua wamepinga uwepo wa Bw Orengo kuwakilisha Bunge la Taifa.

Bw Njiru alisema suala kama hili liliibuliwa wakati wa hoja ya kumtimua aliyekuwa naibu gavana wa Kisii Robert Monda na kwamba mahakama kuu iliamua kuwa mtu aliye katika kazi ya kuajiriwa hawezi kuwakilisha upande wowote mbele ya bunge.

Spika Kingi atafanya uamuzi baada ya Gachagua kusomewa mashtaka.