• Nairobi
  • Last Updated May 7th, 2024 8:11 PM
Akiri kuua mwanawe mchanga kwa kumwamsha kwa kilio

Akiri kuua mwanawe mchanga kwa kumwamsha kwa kilio

MASHIRIKA Na PETER MBURU

MWANAMUME kutoka Utah amekiri kuwa alimpiga mwanawe mchanga ngumi hadi kufa, baada ya mtoto huyo kulia sana usiku hadi vilio vikamwamsha.

Bw Matthew Daniel, 24, alikamatwa miezi 17 iliyopita, kwa kuua mtoto wa wiki nne (mwezi mmoja), aliyeitwa Brayden.

Alikiri mashtaka ya mauaji, ambapo upande wa mashtaka uliitaka korti kutomfunga chini ya kifungo cha miaka 25 gerezani. Kiongozi wa mashtaka aliiomba korti kumfunga maisha.

Bw Daniel aliamshwa na mlio wa alamu pamoja na kilio cha mwanawe mwendo wa saa kumi na mbili na nusu asubuhi, mnamo Septemba 7, 2017, korti ilifahamishwa.

Mshukiwa alikiri kuwa alimpiga ngumi mwanawe kwa hasira alipoamshwa na kilio chake, kisha akamtia mdomoni kifaa cha kumnyamazisha.

Hata hivyo, alisema saa chache baadaye alipokuwa akimpeleka pamoja na mtoto mwingine mahali wanapoachwa watoto mchana, alibaini kuwa hakuwa akipumua.

Mtoto huyo alipofikishwa hospitalini, madaktari walibaini kuwa alikuwa amejeruhiwa sehemu kadha za mwili, hadi akilini.

Wachunguzi katika kesi hiyo walisema mshukiwa, chini ya kiapo, alijitaja kuwa ‘mnyama’.

“Matthew alijitaja kuwa mnyama, kuwa amepoteza imani yote maishani na kuwa atapoteza kila kitu,” zikasema nakala za korti.

Mshukiwa sasa atahukumiwa mnamo Machi 5.

  • Tags

You can share this post!

Kizimbani kwa kumtupia manamke jicho la mapenzi kwa baa

Wanasayansi sasa wadai bangi inaongeza nguvu za kiume

adminleo