Mkuu wa Usalama Ali Larijani aapa Iran haitafanya mazungumzo na Amerika
TEHRAN, Iran
KIONGOZI wa Baraza Kuu la Kitaifa la Usalama nchini Iran Ali Larijani jana alishikilia kuwa “Iran haitafanya mazungumzo na Amerika.”
Kwenye taarifa kupitia mtandao wa X, Larijani alikana madai kwenye baadhi ya vyombo vya habari kwamba maafisa wa Iran walikuwa wameanzisha mazungumzo na utawala wa Trump kufuatia msururu wa mashambulio yaliyotekelezwa nchini humo na wanajeshi wa Amerika na Israel.
Kinaya ni kwamba mashambulio hayo yalijiri baada ya Iran na Amerika kufanya mazungumzo kuhusu mpango wake (Iran) wa utengenezaji zana za nyuklia.
Taarifa ya Larijani, kwenye mtandao wa X ulijiri kujibu ripoti iliyochapishwa na jarida la Wall Street Journal kwamba kiongozi huyo anaendeleza juhudi za kurejelewa kwa mazungumzo na Amerika huku mapigano yakiendelea.