Safari za moja kwa moja kutoka Doha hadi Mombasa zaanza
Shirika la Ndege la Qatar Airways limeanzisha safari za moja kwa moja kutoka Doha hadi Mombasa.
Safari hizo zitaanza kutekelezwa Desemba, katika hatua ambayo inatarajiwa kuzua zaidi ushindani hasa dhidi ya mashirika ya ndege ya humu nchini.
Mombasa ni mji mkubwa zaidi Kenya, baada ya Nairobi, na pia ni mji wa kitalii.
Qatar Airways pia huwa na ziara zake za kawaida kati ya Doha na Nairobi
Huduma hiyo itakuwa ikitolewa mara nne kwa wiki kupitia kwa ndege Airbus A320 na itakuwa ikichukua takriban saa sita kati ya miji hiyo miwili.
Ndege hiyo ina viti 12 za hadhi ya juu (business class) na 120 vya hadhi ya kawaida (economy class).
Ndege zingine ambazo huwa na huduma ya uchukuzi moja kwa moja hadi Mombasa ni Ethiopian Airlines, Turkish Airlines na RwandAir.
Next article
Serikali kuongeza ada ya NHIF