Wanajeshi 100 wa Amerika watua Nigeria kushiriki operesheni
ABUJA, NIGERIA
ZAIDI ya wanajeshi 100 kutoka Amerika Jumanne, Februari 17, 2026 waliwasili Nigeria kuendeleza operesheni kali dhidi ya waasi wa Kiislamu wanaodaiwa kuua Wakristo.
Hii ni baada ya Rais Donald Trump kuteta na kushutumu serikali ya Nigeria kwa kuwavumilia waasi wa Kiislamu wanaoendeleza mauaji dhidi ya Wakristo hasa katika eneo la kaskazini magharibi.
Hata hivyo, Nigeria imekanusha vikali kuwa imekuwa ikipendelea dini yoyote nchini humo.
Mnamo Desemba mwaka jana, Amerika ilishambulia maeneo yanayodhibitiwa na Waislamu.
Pia wanajeshi wa Amerika wamekuwa wakishika doria eneo hilo kuwasaidia wenzao kutoa Nigeria.
Msemaji wa jeshi la Nigeria Samaila Uba alisema kuwa wanajeshi wa Amerika watawapa mafunzo wale wa Nigeria lakini hawatashiriki operesheni dhidi ya makundi yaliyojihami ya Kiislamu.
Mapema mwezi huu jeshi la Nigeria lilisema kuwa lilitarajia zaidi ya wanajeshi 200 zaidi kutoka Amerika.
Msemaji wa Afisi ya Rais Sunday Dare alisema Nigeria inahitaji msaada mkubwa kutoka Amerika.
Hasa alisema wanahitaji ndege za kivita, silaha lakini hakutoa muda ambao vifaa hivyo vitafika Amerika.
Waislamu na Wakristo huwa ni nusu bin nusu kwa idadi yote ya watu milioni 240 kutoka Nigeria. Wakristo huishi kusini huku Waislamu wakitawala eneo la kaskazini.