Raila ataka Ruto alipe familia za Gen Z waliouawa ili nchi isonge mbele
WAZIRI Mkuu wa zamani Raila Odinga ametaka serikali ya Rais William Ruto ilipe familia za waliouawa na kuheruhiwa wakati wa maandamano ya Gen Z mwaka jana ili taifa liweze kusahau na kusonga mbele.
Akizungumza wakati wa sherehe za Madaraka Dei zilizofanyika katika Kaunti ya Homa Bay Juni mosi, Raila alisema lilikuwa jambo nzuri kwamba juzi wakati wa Maombi ya Kitaifa misamaha ilitolewa kuhusu madhila ambayo yametendeka lakini akasema msahama utakubalika iwapo kutafanyika juhudi za kulipa ambao bado wanaumia kutokana na yaliyojiri.
Awali kwenye hotuba yake, Raila alimsihi Rais Ruto kusitisha mienendo aliyosema inaelekea kurejesha utawala wa mikoa akisema mfumo huo wa utawala hauna nafasi katika Kenya ya sasa na chini ya Katiba mpya.