Makala

Jinsi familia ‘ilimzuia’ kwa muda mhubiri Kiuna ‘asiende’ jongomeo

Na FRIDAH OKACHI July 19th, 2024 2 min read

MCHUNGAJI wa Kanisa la Jubilee, Bi Kathy Kiuna afunguka jinsi marehemu mumewe,  Askofu Allan Kiuna alifahamu muda wake kuondoka duniani umewasili. 

Bi Kiuna alisema wakati mwingi mumewe alizungumza kuhusu ‘kwenda nyumbani’ jambo ambalo familia yake na marafiki wa karibu hawakuwa tayari.

“Alijua wakati wake umefika lakini hatukutaka aende. Kila wakati aliniambia kuwa wanamkujia na kujiweka kwenye jukumu la kuwafukuza. Ilifikia wakati hatukutaka aende,” alidokeza Bi Kiuna.

Wakati wa ibada ya mazishi, marehemu alifika kipindi cha kunyamaza kwa kukosa kukubali hali ilivyo.

“Alisema anataka kwenda nyumbani. Na alikuwa akisema mbele yangu na mhubiri Andrew. Nilimsikiza na kumwambia tayari ako nyumbani lakini akawa anasisitiza anataka kwenda nyumbani. Nilichukua jukumu la kumwambia awaambie waende. Kisha akakosa kuendelea kusema hivyo kwa kuwa alikuwa anapambana na maradhi hayo,” alisema Bi Kiuna.

Wakati wa kipindi cha kuugua, Kathy Kiuna alifichua Bw Allan alimwambia kuwa hakupenda marafiki kumtembelea na kila wakati alimhimiza kuwafukuza.

Wakati wa maziko, Bi Kathy Kiuna alimshukuru mumewe kumfunza kuwa mhubiri.

“Mpenzi, sikujua naweza kuwa mhubiri, lakini uliona nina uwezo huo. Ulinihimiza naweza kufanya hili, angalia niliweza kulifanya kutokana na uwezo wa Mungu.”

“Nataka niseme mbele ya umati huu, mpenzi nitazidi kufanya bora zaidi,” aliongeza Bi Kathy Kiuna.

Hata hivyo mama huyo alijivunia uwepo wa mumewe nyakati za dunia baada ya kumfunza kuwa mhubiri na kumchumbia.

“Wakati alinipeleka kwa nabii Teresia Wairimu, nilikuwa na umri wa miaka 24 na hakuniambia ananipeleka huko. Kwa Ufupi, Mama (Teresia) alimwangalia na kumwambia huyu anakufaa. Alikuwa amepeleka wasichana wengine, lakini wote walikataliwa hadi aliponiona,” Bi Kiuna alifumbua.

Bw Kiuna alianza kuugua mwaka wa 2018 na kurejea kwa hali yake ya kawaida baada ya kufanyiwa

upandikizaji wa uboho na kupata nafuu.

Katika mwaka wa 2021, alianza kuhisi maumivu kwenye mguu wake, alitibiwa na kutangaza kuwa huru Novemba 2023 baada ya kupata ripoti ya daktari.

Bi Kiuna alisema alishangaa kuona mumewe kuwa mgonjwa februari 2024,  japo mwezi Machi na Aprili alifanya kazi yake ya huduma katika kanisa lake.