• Nairobi
  • Last Updated April 30th, 2024 8:55 PM
Corona inavyoumiza wafugaji wa kuku

Corona inavyoumiza wafugaji wa kuku

Na KEVIN ROTICH

Kabla kuzuka kwa janga la virusi vya corona, biashara ya kuku ilinoga sana nchini ikilinganishwa na hali ilivyo sasa. Ufugaji pamoja na uagizaji wa kuku wa nyama ulikuwa katika kiwango cha juu kufuatia huduma nyingi katika hoteli na sehemu nyingi za kustarehe.

Biashara hiyo ilipigwa jeki na huduma mpya za usafiri kama vile Uber Eats iliyorahisisha kusambazwa kwa bidhaa na kupunguza muda wa kuwafikia wateja.

Lakini mapema mwaka huu, mambo yalibadilika na kubadili mfumo wa kazi na huduma. Baadhi ya mambo yalioathiri shughuli hizi ni pamoja na kusitishwa kwa safari za ndege, kufungwa kwa mipaka, kupungwa kwa safari pamoja na kafiu wakati wa jioni na usiku.

Idadi ya watu wanaotembelea sehemu mbalimbali pia ilidhibitiwa ili kuzuia maambukizi.

Wafanyibiashara katika kaunti ya Nairobi wanasema hali haijarejea kawaida na itachukua muda kabla ya kazi yao kunawiri tena.

“Wakati huu siwezi kusema hali imerejea kawaida ila ninapata matumaini kila baada ya siku. Wateja si wengi ikizingatiwa kuwa bado kila mtu anachunga usalama wake,” akasema mfanyibiashara mmoja jijini Nairobi.

Wamiliki wa hoteli wanasema wamelazimika kupuguza uagizaji wa kuku kutoka kwa wakulima kufuatia idadi ndogo ya wateja na pia masaa chache ya kufamya kazi.

“Wakati huu viwango vya kuaribika kwa bidhaa viko juu. Mara kwa mara unapata wafanyibiashara wengi wanapata hasara haswa wale wanaonunua na kutayarisha michizi vya kuku,” akasema mfanyibiashara mwingine.

Kulingana naye, hali hapo mbeleni wateja wengi walifurika kwenye mikahawa ambapo wengi waliofika kuchelewa walikosa vyakula walivyoitaji.

Bw Solomon Kinyua ni mmoja wa wakulima walioathirika na kulazimika kupunguza idadi ya kuku aliokuwa akifuga kutoka 30, 000 hadi 2, 000.

Katika shamba lake eneo la Marwa kwnye kaunti ya Nyeri, Bwana Kinyua anasema soko ya kuku wake ilipungua ndiposa akapunguza idadi.

“Naweza kusema soko ilipungua kwa asilimia sitini kutokana na masharti yaliyowekwa na serikali na pia kusitishwa kwa soko la kimataifa kama vile katika nchi za Tanzania na Uganda,” akasema.

Aidha, taifa la Uganda limeongeza ada ya mauzo kwa asilimia 25 kwenye bidhaa za kuku kutoka Kenya, asilimia 18 ya VAT, asilimia sita ya kuzuia kodi na asilimia moja ya ushuru wa barabara.

Kwa mfano, kilo moja ya kuku kutoka taifa la Uganda inauzwa kwa Sh200 ilihali iliotoka Kenya ni Sh300.

Kutokana na hayo, mapato ya Bwana Kinyua yamepungua kutoka Sh6 million hadi Sh400, 000 kwa kila msimu wa miezi miwili wa kufuga. ded

You can share this post!

DJ CUTS: Namshukuru Mola kunifungulia njia ya kuwatumbuiza...

Raha kwa wachuuzi baada ya masoko kufunguliwa