• Nairobi
  • Last Updated March 28th, 2024 11:33 AM
LISHE: Vibibi

LISHE: Vibibi

Na MISHI GONGO

Idadi ya walaji: 6

Viungo

  • vikombe vya unga wa ngano 2
  • hamira kiasi cha kijiko 1/4
  • sukari vijiko vikubwa 3
  • chumvi kiasi cha kijiko cha chai 1/4
  • kikombe cha mafuta ya uto 1/2
  • unga wa sima kikombe 1 1/2
  • iliki tembe 5

Jinsi ya kutayarisha

Ponda iliki yako hadi iwe unga kisha weka pembeni.

Weka hamira kwa kibakuli kidogo, changanya na maji kiasi kisha koroga.

Chukua unga wa ngano, unga wa sima, hamira, sukari, chumvi, na iliki ongeza na maji kiasi kisha changanya hadi mchanganyiko wako uwe uji.

Ongeza kikombe cha maziwa kisha funika mchanganyiko halafu uweke pembeni ukisubiri uumuke.

Unga ukiumuka bandika chuma motoni, teka unga kidogo kidogo ukimwagwa katika chuma cha moto kisha tandaza unga upate umbo la duara.

Choma kwa dakika mbili hadi kibibi kigeuke rangi ya asali. Geuza upande wa chini na ufanye vivyo hivyo.

Kitakapoiva pande zote mbili, epua na uweke kwenye sahani.

Unaweza kula chakula hicho kwa rojo la nyama ya mafuta au kahawa.

You can share this post!

Wanga ataka FKF ihimize na ihamasishe wanasoka kuhusu...

Matunda ya Kazi Mtaani yaonekana mitaa kadhaa Nairobi

adminleo