Shangazi Akujibu

Mtoto niliyepata kabla ya ndoa anateseka, nitamchukuaje?

Na SHANGAZI November 16th, 2025 Kusoma ni dakika: 1

SWALI: Mpenzi wangu aliniacha akaolewa na mwanamume mwingine. Mumewe hana kazi kwa sasa na wanaishi kwa shida. Tulikuwa tumezaa pamoja na nahisi vibaya mtoto wangu akiteseka. Nafikiria kumchukua. Nishauri.

Jibu: Mpango huo utahitaji mazungumzo na maelewano. Ingawa mtoto huyo ni wako kumzaa, sasa ana baba mwingine. Jaribu kushauriana nao bila kugusia hali yao. Itabidi pia uzungumze na mke wako ili amkubali mtoto huyo.

IMETAYARISHWA NA WINNIE ONYANDO