Shangazi Akujibu

SHANGAZI AKUJIBU: Mume humbagua mtoto niliyezaa kabla ya ndoa

Na SHANGAZI December 2nd, 2025 Kusoma ni dakika: 1

SWALI: Kwako shangazi. Niliolewa nikiwa na mtoto kutokana na uhusiano wa awali. Mume wangu aliahidi kumpenda kama wake. Lakini anaonekana kupendelea wawili ambao tumezaa pamoja na hilo linaniumiza moyoni. Nishauri.

Jibu: Mume wako amekiuka ahadi yake kwako. Unafaa umkumbushe na kumwelezea unavyohisi unapoona akimbagua mtoto wako. Kama hatajirekebisha, uko huru kuondoka badala kuendelea kuona mwanao akiteseka.

IMETAYARISHWA NA WINNIE ONYANDO