Shangazi Akujibu
SHANGAZI AKUJIBU: Nilikopa pesa kununua vifaa ili nimuoe, lakini sasa amenikataa
Pesa. PICHA | MAKTABA
SWALI: Shikamoo Shangazi. Nilichukua mkopo ninunue vifaa vya nyumba kabla tuoane lakini mchumba wangu sasa anasema hataki tena mambo ya ndoa. Nimfanyie nini?
Jibu: Usiulize cha kumfanyia. Wewe anza kulipa mkopo, songa mbele na usirudie kosa kama hilo tena.
IMETAYARISHWA NA WINNIE ONYANDO