Shangazi Akujibu

SHANGAZI AKUJIBU:Sijui kupika, nashuku mpenzi wangu atanitema

Na SHANGAZI November 30th, 2025 Kusoma ni dakika: 1

SWALI: Vipi shangazi. Kila nikienda kumtembelea mpenzi wangu, ananilazimisha nimpikie ila mimi sijui kupika. Ninahofia sana ataniacha. Nipe ushauri.

Jibu: Mtu hujifunza kupika, kwa hivyo usitie shaka. Mweleze ukweli wa mambo na uanze kujifunza polepole.

IMETAYARISHWA NA WINNIE ONYANDO