• Nairobi
  • Last Updated May 17th, 2024 6:50 AM
VINYWAJI: Smoothie ya nanasi, ndizi na tangawizi

VINYWAJI: Smoothie ya nanasi, ndizi na tangawizi

Na MARGARET MAINA

[email protected]

Muda wa kuandaa: Dakika 5

Wanywaji: 2

Vinavyohitajika

• vpande vya mananasi yaliyoiva kiasi vikombe viwili

• mdizi mbivu 2

• kikombe ½ cha mtindi

• kijiko 1 cha tangawizi

• vanilla extract kwa kijiko cha chai

• barafu kikombe ½

• shurubati ya nanasi au maji kikombe nusu

Maelekezo

Menya na katakata matunda.

Twanga tangawizi.

Weka viungo vyote kwenye blenda au mashine ya kusagia chakula.

Saga mpaka vilainike.

Mimina kwenye glasi na ufurahie kinywaji.

You can share this post!

Akatwa kwa panga na mwanajeshi akiiba kuku

SIHA NA LISHE: Faida za ubuyu