• Nairobi
  • Last Updated April 30th, 2024 6:55 PM
Kibarua kwa Obiri mita 3,000 Diamond League

Kibarua kwa Obiri mita 3,000 Diamond League

Mkimbiaji Sandrafelis Chebet baada ya kukamilisha mbio za nyika katika uwanja wa Posta kwenye barabara ya Ngong Road, Nairobi. Picha/ Geoffrey Anene

Na GEOFFREY ANENE

MALKIA wa mbio za mita 5,000, Hellen Obiri atakuwa na kibarua kigumu kuanza Riadha za Diamond League za mwaka 2018 vyema baada ya kitengo atakachoshiriki nchini Qatar hapo Mei 4 cha mbio za mita 3000 kuvutia majina makubwa.

Bingwa huyu wa dunia wa mbio za mita 3000 za Riadha za Ukumbini mwaka 2012, ambaye pia anajivunia mataji ya dunia na Jumuiya ya Madola, atakabiliana na bingwa wa dunia wa Mbio za Nyika Agnes Tirop na bingwa wa dunia wa mbio za mita 3000 kwa wakimbiaji wasiozidi umri wa miaka 18 mwaka 2013 Lilian Kasait.

Wakenya wengine katika kitengo hiki ni mshindi wa nishani ya fedha ya mbio za mita 2000 kuruka viunzi na maji mwaka 2015 Sandrafelis Chebet, bingwa wa Afrika wa mbio za mita 3000 kuruka viunzi na maji Norah Jeruto, bingwa wa dunia wa mbio za mita 3000 kuruka viunzi na maji mwaka 2015 Hyvin Kiyeng’, bingwa wa Mbio za Nyika za Afrika mwaka 2011 Caroline Kipkirui na Mary Kuria, ambaye alifika fainali ya mbio za mita 1500 kwenye Jumuiya ya Madola mjini Gold Coast wiki tatu zilizopita.

You can share this post!

Kutazama Elijah Manangoi na nduguye wakimenyana? Utasubiri...

Gathimba kuwania mamilioni Matembezi ya Dunia Uchina

adminleo