• Nairobi
  • Last Updated May 3rd, 2024 7:50 AM
Ratiba ya SportPesa Shield baada ya timu 5 kujiondoa

Ratiba ya SportPesa Shield baada ya timu 5 kujiondoa

Na GEOFFREY ANENE

KLABU za Mathare United, Chemelil Sugar, Zoo Kericho, Thika United na Nakumatt kutoka Ligi Kuu zimesusia mashindano ya soka ya Kombe la Ngao yanayofahamika sasa kama SportPesa Shield.

Sababu ya klabu hizi kutokuwa makini na kombe hili linalotumika kuchagua mwakilishi wa Kenya katika Kombe la Mashirikisho la Afrika (Confederations Cup) haijabainika wazi.

Hata hivyo, burudani hili linatarajiwa kuwa moto baada ya klabu zingine 13 kutoka Ligi Kuu kutoa ithibati ya kushiriki.

Klabu hizo ni AFC Leopards (mabingwa watetezi), Bandari, Tusker, Posta Rangers, Kakamega Homeboyz, Ulinzi Stars, Nzoia Sugar, Vihiga United, SoNy Sugar, Wazito, Kariobangi Sharks, Gor Mahia na Sofapaka.

Mshindi Kombe la Ngao huzoa Sh2 milioni na kuingia Confederations Cup. Leopards inatetea taji ililonyakua baada ya kulipua Kariobangi Sharks 2-0.

Ratiba (SportPesa Shield):

Mwatate United vs Fortune Sacco

Ushuru FC vs Nunguni FC

Bandari FC vs Berlin FC (Garissa)

Tusker FC vs Taita Taveta FC

Leysa FC vs Emmausians (Tana River)

KCB FC vs Nanyuki All Stars

Sofapaka FC vs Re-Union

Equity Bank FC vs Baba Dogo United

Naivas FC vs Friend Zone FC

Zetech University vs Tandaza FC

Gor Mahia FC vs SS Assad (Mombasa)

Savannah Cement FC vs KenPoly FC

Kariobangi Sharks FC vs Nanyuki Youth

Wazito FC vs Nairobi Water FC

Talanta FC vs Ligi Ndogo FC

Modern Coast FC vs Balaji FC

SoNy Sugar FC vs Rain Forest

AFC Leopards vs Shabana FC

GFE 105 vs VegPro FC

Vihiga United FC vs Nyamira All Stars

Kisumu All Stars vs MKU Nakuru

Nakuru All Stars vs River Plate

Kenya Police vs Nakuru West Combined

Nzoia Sugar FC vs Dero FC

Ulinzi Stars FC vs Transmilan FC

Kakamega Homeboyz FC vs ASEC FC

Western Stima FC vs Egerton University

Bidco FC vs Kabras United

Posta Rangers FC vs Transmara Sugar FC

Raiply vs Kisumu Hot Stars

Timsales vs Bungoma Super Stars

Eldoret Youth vs Transfoc

You can share this post!

Wazazi wasaka waganga kutambua wanafunzi wanaochoma shule

Afisa wa Harambee Sacco akana kuiba mamilioni

adminleo