• Nairobi
  • Last Updated May 7th, 2024 9:48 PM
Simbas walia kukosa mshahara wa Novemba

Simbas walia kukosa mshahara wa Novemba

Na GEOFFREY ANENE

TIMU ya taifa ya raga ya wachezaji 15 kila upande almaarufu Kenya Simbas inadai Shirikisho la Raga la Kenya (KRU) mamilioni ya fedha ambayo ni mshahara wa mwezi Novemba mwaka 2018.

Ripoti zinasema kwamba wachezaji 30 waliozuru jiji la Bucharest mnamo Novemba 3 na kujipima nguvu dhidi ya Romania pamoja na kushiriki mchujo wa mwisho wa kufuzu kushiriki Kombe la Dunia kati ya Novemba 11 na Novemba 23 nchini Ufaransa, wanadai KRU Sh40, 000 kila mmoja.

“Tumelipwa marupurupu ya kusafiri nchini Romania na Ufaransa na pia marupurupu ya mechi. Hata hivyo, bado hatujapokea mshahara wetu wa Novemba,” amefichua mchezaji mmoja wa timu hiyo, ambaye hakutaka kutajwa.

Mchezaji huyo tegemeo aliongeza kwamba benchi la kiufundi la maafisa wanane pia halijalipwa kwa muda unaozidi ule wa wachezaji.

Simbas, ambayo ilimaliza Kombe la Afrika katika nafasi ya pili nyuma ya Namibia mwezi Agosti, ilichabangwa 36-5 na Romania kabla ya kulemewa na Canada (65-19), Hong Kong (42-17) na Ujerumani (43-6). Canada ilipepeta kila timu katika mchujo huo na kunyakua tiketi ya kushiriki Kombe la Dunia nchini Japan.

You can share this post!

Liverpool hawakamatiki baada ya kuitia adabu Arsenal

Mashabiki waitaka Ingwe iwagware Rangers kukomesha matokeo...

adminleo