Habari Mseto

Muuza nguo aliyetapeli benki Sh9.1 milioni  

Na RICHARD MUNGUTI August 23rd, 2024 1 min read

MUUZAJI nguo River Road Nairobi ameshtakiwa kwa wizi wa zaidi ya Sh9 milioni za EcoBank tawi la Westlands, Nairobi.

Lakini Jeremiah Anakoli Amoyo aliyekana mashtaka mawili dhidi yake alieleza mahakama, “Mimi sikuiba hata. Hakuna hata senti moja ilipotea. Pesa zote ziko kwa benki.”

Amoyo alikana kuiba Sh9, 113, 748 za Eco-Bank miezi mitano iliyopita kati ya Feburuari 1-5, 2024.

Shtaka la pili lilisema mnamo Feburuari 1, 2024 alipokea katika akaunti yake kimaksudi kima cha Sh9, 113, 748 zilizotumwa kimakosa kutoka kwa akaunti ya Veka Plaza Limited.

Amoyo alimsihi hakimu mkuu Susan Shitubi amwachilie kwa dhamana isiyo ya kiwango cha juu akisema “hana mapato ya juu.”

Mshtakiwa alieleza mahakama kwamba kwa mwezi hupata tu Sh30, 000 na dhamana inayozidi Sh200, 000 hataweza kuilipa.

Akitoa uamuzi kuhusu dhamana, Bi Shitubi alimwachilia kwa dhamana ya Sh500, 000 pesa tasilimu.

Kesi itatakwa baada ya wiki mbili.

[email protected]