• Nairobi
  • Last Updated April 20th, 2024 10:55 AM
‘Ukeketaji bado unaendelea Embu’

‘Ukeketaji bado unaendelea Embu’

NA CHARLES WANYORO

Wasichana wanne waliokeketwa Kaunti ya Embu Kijiji cha Gitugi wameruhusiwa kwenda nyumbani kutoka hospitalini na kupelekwa kwa nyumba spesheli ili kupewa nasaha. 

Wasichana hao watajiunga na wenzao walionusuriwa wakiwa wanatayarishwa kukeketwa. Ukeketaji huo uliendeshwa na wauguzi waliostaafu.

Diwani mteule Sicily Warue alisema kwamba wanaendelea kuchunguza jinsi wasichana hao wanavyoendelea, ambao wana umri kati ya miaka 8 na 12.

Bi Warue alisema kwamba watatunga sheria itakayosaidia kumaliza ukeketetaji wa wasichana wa shule.

Madiwani ambao ni wanachama wa kamati ya jinsia, utamaduni, watoto na huduma za jamii walisema kwamba vitendo hivyo vilivyopitwa na wakati vilikuwa bado vinatekelezwa katika kaunti hiyo kwa sababu ya kukosa sheria  zitakazochukuliwa dhidi ya ngariba.

Huku akiongea baada ya kutembelea hospitali hiyo ya Embu, Bi Warue alisema kwamba kamati itatengeneza sheria itakayoeleza adhabu itakayochukuliwa wakeketaji hao wa zamani. Diwani huyo alisema atawahimiza madiwani wote wanawake waunge mkono mswada huo.

Bi Warue alisema kwamba madiwani wanaume waliahidi kuhakikisha kwamba mswada huo umepitishwa.

Diwani mteule Elizabeth Kibai aliwahimiza pia wenzake waunge mkono mswada huo ili kuokoa wasichana kutokana na unyama huo.

You can share this post!

Aponea kifo akivuka mto watu 20 wakifariki

Prof Kiama aanza kazi rasmi Chuo Kikuu cha Nairobi

adminleo