• Nairobi
  • Last Updated April 26th, 2024 7:00 PM
I&M pia yapungukiwa na faida

I&M pia yapungukiwa na faida

Na BERNARDINE MUTANU

BENKI ya I&M imepata upungufu wa mapato yake baada ya kutozwa ushuru kwa asilimia sita, katika mwaka uliokamilika Desemba 31, 2017.

Kampuni hiyo ilipata Sh9.9 bilioni baada ya kutozwa ushuru ikilinganishwa na Sh10.6 bilioni katika kipindi hicho mwaka uliotangulia.

Kulingana na kampuni hiyo, hilo lilishuhudiwa hasa kutokana na changamoto za zilizoshuhudiwa nchini kwa sababu ya siasa na kudhibitiwa kwa viwango vya riba na Benki Kuu ya Kenya.

Mwenyekiti wa IMHL Daniel Ndonye alisema Jumanne alisema benki hiyo inaunga mkono viwango vipya vya kimataifa vya kifedha (IFRS 9) kutokana na kuwa iliamini kuwa viwango hivyo vitaweza kuimarisha hali.

Alisema kampuni hiyo imetenga Sh4.1 bilioni kukabiliana na changamoto katika baadhi ya sekta katika operesheni zake zilizoonekana kuathirika vibaya.

You can share this post!

Kampuni 5 zanufaika na malipo ya chini forodhani

Diwani akanusha mashtaka 6 ya ulaghai Murang’a

adminleo