• Nairobi
  • Last Updated March 28th, 2024 11:33 AM
Kibra Girls yawaka moto ligi ya KWPL ikielekea ukingoni

Kibra Girls yawaka moto ligi ya KWPL ikielekea ukingoni

NA RUTH AREGE

TIMU ya Kibra Girls Soccer imepanda hadi nafasi ya kwanza kwenye jedwali la kundi A baada ya kuwapepeta Mombasa Olympic mabao 7-0 katika mechi ya Ligi Kuu ya Wanawake KWPL divisheni ya kwanza.

Kufuatia ushindi huo, Kibra wanaongoza jedwali kwa alama 43.

Mathare Women wanafuata katika nafasi ya pili kwa alama 40. Nao Mombasa Olympic wanavuta mkia kwa alama 12.

MTG United kutoka kaunti ya Kilifi huenda wakarejea ligi kuu ya wanawake msimu ujao baada ya ushindi wao wa 3-1 dhidi ya Sunderland Samba wikendi iliyopita. MTG walipanda hadi nafasi ya pili wakiwa na alama 42 nao Samba wakashuka hadi nafasi ya sita wakiwa na pointi 21.

Gusii Starlets walipata ushindi wao wa pili msimu huu baada ya kuwazidi nguvu Nyuki Starlets kwa mabao 2-0. Ushindi huo umewapandisha hadi nafasi ya nane wakiwa na alama tano nao Nyuki wamesalia kwenye nafasi ya saba kwa alama 14.

Solasa Women walishindwa kutamba nyumbani walipowaalika Gideon’s Starlets mechi ambayo ilikamilika kwa sare ya 1-1. Solasa walipoteza alama mbili ambazo zingechupisha hadi nafasi ya pili kwenye jedwali. Baada ya mechi hiyo, Starlets walisalia katika nafasi ya pili na alama 23 nao Solasa wakabakia katika nafasi ya tatu wakiwa na alama 20.

Royal Starlets walishindwa kupata alama tatu muhimu baada kukabana koo 2-2 dhidi ya Oserian Ladies.

Starlets ambao wanaongoza jedwali kwa alama 23 wanapata ushindani mkubwa kutoka kwa Gideon’s na Solasa Women ambao wanashikilia nafasi ya pili na tatu mtawalia katika kundi B.

Mechi kati ya Ukunda Starlets na Soccer Sisters haikumalizika baada ya timu ya nyumbani Ukunda kushindwa kutimiza hitaji la kutoa huduma ya ambulensi.

Mechi hiyo ilitamatika kipindi cha kwanza baada ya Sisters kususia kucheza.

Sisters walipewa alama tatu na mabao mawili.

Falling Waters Barcelona walivuna ushindi wa 4-1 dhidi ya Uweza Women.

Ushindi huo uliwakweza hadi nafasi ya tano na alama 23 huku Uweza wakisalia katika nafasi ya nne na alama 32.

Vihiga Leeds walidondoka hadi nafasi ya tisa na alama tano baada ya sare ya 1-1 dhidi ya Bungoma Queens.

Msimu huu huenda wasishuke daraja baada ya timu tatu zikiwemo Bomet Starlets, Bomet na SEP Oyugis kushushwa daraja mapema msimu huu.

  • Tags

You can share this post!

Kocha Mwalala apigwa kalamu Homeboyz FC

Shule za kibinafsi sasa tayari kwa CBC ya sekondari

T L