• Nairobi
  • Last Updated April 26th, 2024 7:00 PM
Kijana, 20, aondolewa kesi ya ubakaji baada ya kudhihirisha alikuwa mpenzi wa siri wa mlalamishi, 48

Kijana, 20, aondolewa kesi ya ubakaji baada ya kudhihirisha alikuwa mpenzi wa siri wa mlalamishi, 48

KNA na LABAAN SHABAAN

MWANAMUME wa umri wa miaka 20 ameshusha pumzi baada ya mahakama ya Loitoktok kumuondolea shtaka la ubakaji.

Loshipa Papaiyo alifika mbele ya Hakimu Mkuu Judicaster Nthuku kujibu shtaka la ubakaji aliloshukiwa kutenda mnamo Aprili 20, 2023.

Mshukiwa huyo alituhumiwa alimbaka mwanamke wa umri wa miaka 48 eneo la Inchakita, Kaunti ndogo ya Loitoktok.

Wakiwa kortini, mlalamishi aliambia mahakama tukio lilifanyika alipokuwa kichakani akichanja kuni.

Mwanamke huyo alisema mshukiwa, ambaye alikuwa anachunga mifugo, alimparamia na kumkaba shingoni akimtisha asipige kelele.

Mlalamishi aliripoti kuwa mwanaume huyo alimtisha angemuua kama angepiga mayowe.

Anadai kwamba baina ya mayowe, mshukiwa alimbaka kabla ya kutoroka alipofumaniwa na mhudumu wa bodaboda.

Alidokeza kuwa ni bodaboda alitafuta usaidizi ulioishia kuanzishwa kwa msako wa mshukiwa.

Mchungaji alikamatwa msituni humo na kupelekwa hadi kituo cha polisi cha Mbirikani kisha kushtakiwa kwa ubakaji.

Lakini, mshukiwa alikana madai ya ubakaji akisema walifahamiana na mlalamishi ambaye aliridhia tendo la ndoa.

Kadhalika, alifichua kwamba walikuwa na mapenzi ya kisiri kwani mlalamishi alikuwa ameolewa.

Aliendelea kuthibitishia mahakama walivyokutana nyumbani mwa mwanamke huyo ili kurusha roho mume alipoondoka.

Korti ilidhihirisha haya kuwa kweli kwa wakati mshukiwa alifaulu kueleza mpangilio wa nyumba hiyo.

Ikimuondolea lawama ya ubakaji, korti ilimkosoa mwanamke kwa kudai hawakufahamiana na mshukiwa.

Idara ya haki ilitambua wawili hawa walikubaliana kukutana msituni kwa sababu mume alikuwa nyumbani.

Na walipofumaniwa na mhudumu wa bodaboda, mlalamishi alimruka mshukiwa na kusema alibakwa.

Korti iliamua upande wa mashtaka haukuweza kudhihirisha kikamilifu shtaka la ubakaji na hivyo ikamwondolea kesi.

  • Tags

You can share this post!

Nilikunywa glasi moja pekee ya chang’aa nikaishia...

Hawara achomea picha vidume wa Man U akidai wote ni mafisi...

T L