• Nairobi
  • Last Updated April 24th, 2024 8:50 AM
Kimetto kushiriki Boston Marathon baada ya miaka minne

Kimetto kushiriki Boston Marathon baada ya miaka minne

Na GEOFFREY ANENE

MSHIKILIZI wa rekodi ya dunia ya mbio za kilomita 42 ya wanaume, Dennis Kimetto, ametangaza atashiriki Boston Marathon nchini Marekani mnamo Aprili 16, 2018.

Kimetto, ambaye anajivunia kasi ya juu kuwahi kutambuliwa na Shirikisho la Riadha duniani (IAAF) katika mbio hizi ya saa 2:02:57, hajakuwa akionekana tangu aweke rekodi hiyo katika Berlin Marathon nchini Ujerumani mwaka 2014.

Mwaka 2015, aliwakilisha Kenya katika Riadha za Dunia jijini Beijing nchini Uchina, lakini hakukamilisha mbio.

Alijiondoa kushiriki Chicago Marathon nchini Marekani mwaka 2016 kwa sababu ya kujeruhiwa mguu wake wa kushoto.

Kimetto aliapa kuvunja rekodi hiyo ya dunia katika Chicago Marathon mwaka 2017, lakini hakufanikiwa kumaliza makala hayo. Alijiondoa kabla ya kukamilisha kilomita 25.

“Nahisi niko na nguvu sasa kutokana na mazoezi nimekuwa nayo tangu mwaka jana (2017). Natumai nitarejea kwa kishindo mjini Boston,” Kimetto, ambaye alianza kushiriki mbio za kilomita 42 mwaka 2012, aliambia gazeti la Daily Sport.

You can share this post!

Esperance ya Tunisia yatua nchini kuchuana na Gor Machakos

Mng’oa meno aamriwa asikizane na shemeji zake

adminleo