• Nairobi
  • Last Updated March 29th, 2024 7:50 AM
Kizaazaa benten akitaka kula kuku na vifaranga wake

Kizaazaa benten akitaka kula kuku na vifaranga wake

NA JANET KAVUNGA

MALINDI MJINI

MUMAMA mmoja mjini hapa alimtimua benten aliyekuwa amemweka kinyumba, barobaro huyo alipoanza kumnyemelea binti yake.

Kwa miaka miwili, jamaa alikuwa akitunzwa na mama huyo hadi juzi, binti anayeishi majuu alipomtembelea mama yake.

Jamaa alitekwa na urembo na umbo la demu huyo hadi akashindwa kujizuia kumrushia mistari.

Demu hakuamini jamaa akimtongoza ilhali alikuwa mpenzi wa mama yake na akamkemea vikali barobaro huyo kwa kukosa heshima.

Habari zilipofikia mumama, alikasirika na kumtimua jamaa kutoka nyumba yake huku akimtishia vikali kwa kutaka kutafuna kuku na kifaranga wake.

  • Tags

You can share this post!

Wafanyabiashara wajenga vibanda visivyotakikana wakidai...

Raila achamba serikali kwa kuuzia wakulima ‘mbolea ya...

T L