NA JANET KAVUNGA
MALINDI MJINI
MUMAMA mmoja mjini hapa alimtimua benten aliyekuwa amemweka kinyumba, barobaro huyo alipoanza kumnyemelea binti yake.
Kwa miaka miwili, jamaa alikuwa akitunzwa na mama huyo hadi juzi, binti anayeishi majuu alipomtembelea mama yake.
Jamaa alitekwa na urembo na umbo la demu huyo hadi akashindwa kujizuia kumrushia mistari.
Demu hakuamini jamaa akimtongoza ilhali alikuwa mpenzi wa mama yake na akamkemea vikali barobaro huyo kwa kukosa heshima.
Habari zilipofikia mumama, alikasirika na kumtimua jamaa kutoka nyumba yake huku akimtishia vikali kwa kutaka kutafuna kuku na kifaranga wake.