• Nairobi
  • Last Updated April 19th, 2024 1:14 PM
Lautaro Martinez aongoza Inter Milan kupepeta Fiorentina na kunyanyua taji la Coppa Italia

Lautaro Martinez aongoza Inter Milan kupepeta Fiorentina na kunyanyua taji la Coppa Italia

Na MASHIRIKA

LAUTARO Martinez alifunga mabao mawili katika ushindi wa 2-1 dhidi ya Fiorentina na kusaidia waajiri wake Inter Milan kutoka nyuma na kunyanyua taji la Coppa Italia kwa mara ya pili mfululizo.

Fiorentina walitangulia kuona lango la Inter kunako dakika ya tatu kupitia kwa Nico Gonzales katika mechi hiyo iliyosakatiwa ugani Olimpico.

Hata hivyo, Martinez alisawazisha kunako dakika ya 29 kabla ya kupachika wavuni goli la pili na la ushindi dakika nane baadaye.

Fiorentina wanajiandaa sasa kuvaana na West Ham United katika fainali ya Europa Conference League mnamo Juni 7, 2023, siku tatu kabla ya Inter kuvaana na Manchester City kwenye fainali ya Klabu Bingwa Ulaya (UEFA) jijini Istanbul, Uturuki mnamo Juni 10, 2023.

TAFSIRI NA: CHRIS ADUNGO

  • Tags

You can share this post!

Rais Ruto ampiga Raila chenga

Waziri Machogu kuzindua rasmi kituo cha maji safi shuleni...

T L