• Nairobi
  • Last Updated April 18th, 2024 11:55 AM
Mbogo adai Nassir hana rekodi nzuri ya kutekeleza miradi

Mbogo adai Nassir hana rekodi nzuri ya kutekeleza miradi

NA MWANDISHI WETU

MBUNGE wa Kisauni, Ali Mbogo, amemsuta mwenzake wa Mvita amekosoa azma ya mwenzake wa Mvita, Abdulswamad Nassir ya kuwania ugavana wa Mombasa.

Kulingana na mbunge huyo, Bw Nassir hakuzindua miradi ya maendeleo katika kipindi cha miaka 10 ambayo amekuwa mbunge, hivyo hawezi kutegemewa kuinua Mombasa kimaendeleo.

“Tuambieneni ukweli. Nassir amekuwa mbunge kwa miaka 10 na hakuna maendeleo aliyoyaleta Mvita. Sasa vile yuataka kuwa gavana, ataweza kusaidia Mombasa kimaendeleo?” akauliza Bw Mbogo alipowahutubia wakazi wa Mjambere alipokuwa akijipigia debe la kutaka kuwania ugavana wa Mombasa.

Mwingine ambaye ametangaza atawania cheo hicho ni mfanyibiashara ni Suleiman Shahbal.

Kulingana na Bw Mbogo, kwa miaka minne ambayo amekuwa mbunge wa Kisauni amefanikiwa kujenga shule tano mpya.

Aliwataka wakazi wamchague kama mrithi wa Gavana Hassan Joho ili afanikishe maendeleo katika maeneo mengine yote ya Mombasa.

“Ugavana si kazi ndogo. Angalieni vile nimebadilisha Kisauni. Jamaa wa Mvita atuonyeshe shule alizojenga kwa miaka 10 akiwa uongozini. Halafu unaskia mtaani watu wakisema wanampa ugavana, munampa kwa msingi gani?” aliuliza.

Bw Mbogo, ambaye ni mwanachama wa Wiper, alisema ataendeleza miradi ya maendeleo ili kusaidia watoto wa familia maskini.

  • Tags

You can share this post!

Mvurya atengewa cheo katika upeo wa Kenya Kwanza

Mkenya anayetakiwa Rwanda kutumikia kifungo cha miaka...

T L