• Nairobi
  • Last Updated March 29th, 2024 6:25 PM
Mfungwa akiri kumlaghai mwanamke Sh0.8Milioni kumsaidia kupata kazi ikulu ya Nairobi

Mfungwa akiri kumlaghai mwanamke Sh0.8Milioni kumsaidia kupata kazi ikulu ya Nairobi

Na Richard Munguti

MFUNGWA anayetumikia kifungo cha maisha amerudishwa akikabiliwa na shtaka la kumlaghai mwanamke Sh0.8milioni akimdanganya atamtafutia kazi katika Ikulu ya Nairobi.

Patrick Shikure Amere alikiri alimlaghai Dkt Selina Vukinu Ambe aliposhtakiwa mbele ya hakimu mkuu mahakama ya Milimani Bi Wendy Kagendo. Shikure alikiri alipokea pesa hizo kwa simu yake kupitia mtandao wa Mpesa. Hata hivyo Shikure hakuhukumiwa baada ya kukiri shtaka la kumlaghai Dkt Ambe ila alirudishwa gerezani hadi Feburuari 22,2022 atakapoadhibiwa.

Na wakati huo huo Bi Kagendi alimwamuru Mkurugenzi wa Uchunguzi wa Jinai (DCI) achunguze jinsi wafungwa hupata simu wanazotumia kuwafuja wananchi pesa kwa njia ya mtandao. Akieleza jinsi Dkt Ambe alitapeliwa kiongozi wa mashtaka Anderson Gikunda alisema mshtakiwa alitumia mtandao wa Facebook na Whatsapp.

Bw Gikunda alisema mshtakiwa alipokea pesa hizo na mlalamishi hakupata kazi hiyo

You can share this post!

Jitihada ni madini

Mabawabu watatu wakana wizi wa vifaa kutoka hospitali

T L