• Nairobi
  • Last Updated March 18th, 2024 8:55 PM
Museveni aahidi kujali zaidi maslahi ya maskini

Museveni aahidi kujali zaidi maslahi ya maskini

Na Eriasa Mukiibi Sserunjogi

RAIS Yoweri Museveni ameapa kuwapa kipaumbele maskini katika jamii anapoingia mamlakani tena, badala ya kusimamia utawala ambao hunufaisha mabwanyenye wachache nchini.

Aliahidi kuhakikisha elimu bila malipo, huduma za matibabu bila malipo katika hospitali za umma na kujitahidi kuimarisha sekta ya uchumi nchini humo katika soko la ulimwengu.

Alikuwa katika hali ya kivita huku akivalia koti lake la kijeshi wakati wote mnamo Jumamosi usiku alipokuwa akihutubia taifa hilo saa kadha baada ya kutangazwa mshindi katika uchaguzi wa Januari 14.

Wahudumu wa Rais wanasema Rais anapovalia magwanda ya kijeshi, huwa wanajua mambo si kama kawaida na kwamba amekasirika.Museveni alisema tatizo moja sugu nchini Uganda limekuwa udanganyifu katika chaguzi, ambao alisema hufanywa kupitia kujaza masanduku ya kura, kupiga kura mara kadhaa na mbinu nyinginezo.

Alisema uhalifu huo ulipunguzwa pakubwa na mashine za utambulishaji zilizotumiwa katika uchaguzi wa hivi punde nchini humo.

 

You can share this post!

Jubilee inanidhulumu, alia mwaniaji ubunge Kabuchai

Facebook yazima ujumbe wa Uhuru kwa Museveni