• Nairobi
  • Last Updated April 26th, 2024 7:00 PM
Padre afutwa kazi kwa kukataa kuoa

Padre afutwa kazi kwa kukataa kuoa

WAUMINI wa kanisa la ACK St John, Othaya, Kaunti ya Nyeri jana walifanya ibada kwenye lango la kanisa baada ya padre wao kufutwa kazi kwa kukataa kuoa.

Padri huyo John Gachau alijipata njia panda baada ya washiriki wanaompenda kumwendea nyumbani kwake na kumsindikiza hadi kanisani na kumtaka awaongoze kwa ibada.

Hii ilikuwa kinyume na maagizo ya mkubwa wake, Askofu Joseph Kagunda anayesimamia dayosisi ya Mlima Kenya Magharibi, kwamba aache kazi ya kuhubiri kwa kuwa hajaoa.

Askofu Kagunda alimpatia Padri Gachau makataa ya miezi sita atafute mke au apoteze kazi yake kama kiongozi wa kanisa akikosa kufanya hivyo.

Muda huo ulipopita Desemba, Askofu Kagunda alimwandikia barua kukumbusha makubaliano yao kuhusu hali yake ya ndoa na akamwagiza aache kazi kuanzia Januari 1, 2022.

Lakini washiriki walimtetea Bw Gachau, wakisema alikuwa akidhulumiwa bila sababu. Jana, waliandamana kutoka nyumbani kwake na kumpeleka kanisani wakitaka awahubirie.

Wakibeba mabango yenye maandishi: “Wake hawanunuliwi katika maduka’, waumini hao waliimba na kucheza densi wakimpeleka kanisani mitaa 500 kutoka kwake. Katika lango la kanisa walimtaka Gachau aendelee kuwahudumia kama padri wao.

  • Tags

You can share this post!

Equatorial Guinea yaning’iniza Algeria pembamba...

Shujaa roho juu ikielekea Malaga 7s Uhispania

T L