• Nairobi
  • Last Updated March 29th, 2024 9:50 AM
Tammy Abraham atua Italia kukamilisha uhamisho wake hadi AS Roma kwa Sh5.3 bilioni

Tammy Abraham atua Italia kukamilisha uhamisho wake hadi AS Roma kwa Sh5.3 bilioni

Na MASHIRIKA

FOWADI Tammy Abraham wa Chelsea ametua nchini Italia kufanyiwa vipimo vya afya na kukamilisha uhamisho wake hadi kambini mwa AS Roma kwa Sh5.3 bilioni.

Kikosi cha Roma kinachonolewa na kocha Jose Mourinho, kimekuwa kikimhemea Abraham ili ajaze pengo la Edin Dzeko aliyesajiliwa na Inter Milan ambao pia walijipata katika ulazima wa kujaza nafasi iliyoachwa na Romelu Lukaku aliyerejea Chelsea kwa Sh15.2 bilioni.

Kwa mujibu wa mkataba ambao Abraham anatarajiwa kutia saini kambini mwa Roma, Chelsea watakuwa na fursa ya kumsajili upya fowadi huyo raia wa Uingereza kwa Sh10.6 bilioni kuanzia 2023.

Abraham, 23, alikuwa mfungaji bora wa Chelsea katika kampeni za 2020-21 na alinolewa na Mourinho kwa misimu miwili katika kikosi cha watu wazima kambini mwa Chelsea baada ya kukwezwa daraja kutoka kikosi cha akademia.

TAFSIRI NA: CHRIS ADUNGO

You can share this post!

Kocha Brendan Rodgers amtunuka sifa fowadi Jamie Vardy

Benzema aongoza Real Madrid kuzamisha chombo cha Alaves...